Malengo 17 ya Dunia

Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu Dunian

lengo la pili

 

Lengo La Pili: Kuondo njaa. Kuwa na Usalama wa Chakula. Kuboresha hali ya Lishe na kukuza Kilimo Endelevu Kidunia Wastani wa Watoto wenye lishe Duni imepungua kwa takribani nusu yake toka mwaka 1990; kutoka asilimia 12.9 kwa mwaka 2014-2016. Hata hivyo kati ya watu 9, mtu mmoja duniani kote, sawa na watu milioni 795 bado ana lishe Duni.
Sehemu kubwa duniani ya watu wasiokuwa na chakula wanaishi katika nchi zinazoendelea, ambako asilimia 12.9 ya watu wake wanalishe Duni. Bara la Asia ndilo lenye idadi kubwa ya watu wenye njaa, Ikiwa ni theluthi mbili za idadi ya watu wenye njaa Duniani. Idadi ya watu wenye njaa Kusini mwa Asia imekuwa ikipungua katikati miaka ya karibuni lakini Mangharibi mwa Asia idadi imeongezeka kidogo. Nchi za Kusini mwa jangwa la Sahara, Barani Afrika lenye kiwango kikubwa cha kutapakaa (wastani wa idadi ya watu) kwa njaa. Hapa katikati kila watu wanne mtu mmoja analishe Duni. Lishe duni inasababisha karibu nusu (Sawa na asilimia 45) ya Vifo vya Watoto chini ya miaka mitano, sawa na watoto milioni 3.1 Kila Mwaka.
Mtoto mmoja kati ya watoto wanne duniani anakabiliwa na tatizo la Udumavu. Katika nchi zinazoendelea idadi yake imeongezeka na kuwa, Kati ya watoto watatu mmoja ana Udumavu Takribani Watoto Milioni 66 wa shule za msingi huhunduria madarasa wakiwa na njaa, na Afrika pekee ina watoto wa aina hiyo milioni 23. Kilimo ndicho kinacho toa sehemu kubwa ya ajira Duniani, asilimia 40 ya watu duniani hutegemea kilimo kwa maisha yao. Na hii ndiyo sekta kubwa inayoajiri kaya Masikini Vijijini Kuna Mashamba madogo milioni 500 duniani kote, mengi yakitegemea kilimo cha mvua, yakitoa asilimia 80 ya chakula kinachotumika duniani hasa katika nchi zinazoendelea. Kuwekeza kwa wakulima wadogo ndio njia bora ya kuhakikisha kuwapo kwa usalama wa chakula kwa mahitaji ya ndani na soko la Dunia

No comments

Theme images by jangeltun. Powered by Blogger.